Thursday 10 July 2014

Watu-72-wauawa-katika-mashambulizi-ya-ukanda-wa-gaza.


SAMEXA.BLOGSPORT.COM
Mashambulizi ya angani ya jeshi la Israel yameendelea usiku kucha katika Ukanda wa Gaza, na kuongeza idadi ya vifo vya Wapalestina kufikia 72 tangu mashambulizi hayo yalipoanza Jumanne wiki hii.(Martha Magessa)
Mashambulizi hayo yanawalenga wanamgambo wa Hamas katika Ukanda wa Gaza ambao nao wameyavurumisha makombora katika taifa hilo la Kiyahudi.
Mjumbe wa Palestina katika Umoja wa Mataifa, Riyad Mansoor ametoa wito wa kuitishwa kikao cha dharura cha Baraza la Usalama ili kuijadili hali hiyo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ameyaalani mashambulizi ya maroketi yanayofyatuliwa kutoka Gaza hadi Israel akisema hayakubaliki na lazima yakomeshwe.
Pia amemtaka Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kujizuia na kuheshimu wajibu wa kimataifa wa kuwalinda raia.
Ban anatarajiwa kuuhutubia mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama hii leo kuhusiana na mzozo huowa Mashariki ya Kati.
CHANZO:DW

Tuma Maoni 0718192930, E-mail samexavery@yahoo.com

No comments:

Post a Comment