Thursday 11 September 2014

Zitto: Sina, sipendi, wala sitegemei kufanya biashara

    
  Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akifafanua jambo.

Ni mengi yamesemwa kuhusu mwanasiasa huyu kijana ambaye ameongoza harakati za kisiasa katika chama chake, Chadema kwa mafanikio, ingawa safari yake ndani ya chama hicho inaelekea kuishia mahali pasipo salama. Pia, ameongoza kamati muhimu za Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa mafanikio makubwa.  Katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Zitto ana lipi la kueleza?
Swali: Hivi ukiacha siasa unatarajia kufanya shughuli gani?
Jibu: Mimi ni mchumi na mtakumbuka baada ya hoja ya Buzwagi mwaka 2007, kamati ya Jaji Bomani  (Mark) 2007/08 tulivyo-submit (wasilisha), ripoti ya Bomani iligundua kwamba sina maarifa ya kutosha kwenye uchumi wa madini, hivyo nikaamua kwenda kusoma Ujerumani Masters ya pili ya Law in Business (Shahada ya Uzamili ya Sheria za Biashara), nikiwa bado mbunge mwaka 2009/10.
Katika Masters ile andiko langu lilihusu mfumo wa kodi kwenye sekta ya madini, mafuta na gesi. Kwa hiyo nimekuwa nikifanya chambuzi mbalimbali kama huu nilioufanya leo na kutumika katika gazeti dada la Mwananchi, The Citizen kuonyesha ni kiwango gani cha mapato ambacho Tanzania itapoteza katika kipindi cha miaka 15 ya uchimbaji wa gesi, ambayo ni Dola 55 bilioni ambayo ni zaidi ya mara mbili ya uchumi wa Tanzania.
Kwa hiyo, ninashiriki katika hizo professional associations (vyama vya kitaaluma), mimi sina biashara na sijui biashara na sina interest (nia) na biashara. Kazi ninayoipenda ni kufanya chambuzi na kufundisha.
Nimeombwa na mmoja wa maprofesa Chuo Kikuu Dar es Salaam kumsaidia katika darasa lake la Masters ya International Trade, pili Chuo cha Taifa cha Masuala ya Ulinzi (National Defense College) kule Kunduchi nimehadhiri kwenye masuala haya ya madini, gesi na mafuta.
Swali: Vipi kuhusu familia, umeoa na una mtoto?
Jibu:  Nina mtoto mmoja lakini sijaoa. Mtoto wangu anaitwa Chachage na nilimwita jina hilo kwa sababu Chachage (Profesa Sethy, marehemu) alikuwa mwalimu wangu Chuo Kikuu na alifariki Julai, 2006 na mtoto wangu alizaliwa Novemba 2006.
Mimi ni mjamaa kiitikadi. Watu wangu ni kina Chachage na Profesa Issa Shivji. Tangu nikiwa chuo, Profesa Shivji anafundisha sheria, lakini most of the time (muda mwingi) niko ofisini kwake wakati mimi nilikuwa nasoma uchumi. Chachage alikuwa anafundisha sosholojia.
Sababu inayonifanya nisioe mpaka sasa ni kutotaka kuanza kujenga familia yangu wakati nina jukumu la kuhakikisha wadogo zangu wanalelewa properly (vyema).
Swali: Marehemu mama yako (Shida Salum) amewahi kukushauri kuacha siasa na ufanye kazi unayoipenda ya kufundisha, ushauri huu unauzingatia vipi?
Jibu: Mama ni mama, mama alikuwa anajua jinsi nilivyojitoa kuhakikisha Chadema inakuwa mpaka hapa ilipofikia kwa hiyo alipokuwa akiona migogoro ile na anajua kabisa kwamba these people are not fair (watu hawa hawakunitendea haki) kwa mwanangu kwa nini sasa mwanangu apoteze muda wake kwa watu ambao hawajali kazi alizofanya.
imeandikwa katika gazeti pendwa la mwananchi....reported by sam exavery.

No comments:

Post a Comment