Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo
Filikunjombe kushoto akishirikiana na mwananchi wa Lupingu kukata mti
uliokuwepo katika njia ya kupitisha umeme kutoka Ludewa kwenda Lupingu
baada ya mbunge huyo kushinda siku nzima akishiriki maendeleo ya
kupeleka umeme Lupingu jumla ya vijiji 49 Ludewa kupelekewa umeme
Mbunge
Filikunjombe wa pili kulia akimsikiliza mwakilishi wa meneja wa
Tanroads mkoa wa Njombe Bw KIndole wakati akielezea maendeleo ya ujenzi
wa barabara Ludewa
MBUNGE wa
jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe amepania kutumia dakika zake 15
bungeni kuwalipua makandarasi wabovu wanaoendelea na ujenzi wa barabara
mbali mbali katika wilaya ya Ludewa ikiwemo barabara ya Njombe -Ludewa
na Ludewa - Manda(Martha Magessa)
Mbunge
huyo alitoa kauli hiyo juzi wakati akikagua ujenzi wa barabara hizo
katika wilaya ya Njombe na kuwa katika baadhi ya maeneo hajafurahishwa
na utendaji kazi wa kampuni husika kutokana na kufanya kazi hiyo chini
ya kiwango na kuwa hadi sasa ni kampuni moja pekee ambayo imeonyesha
kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa .
"
Serikali imewekeza mabilioni ya shilingi katika ujenzi huu wa barabara
katika wilaya ya Ludewa na lengo likiwa ni kusaidia wananchi kuondokana
na adha ya ubovu wa barabara .....sasa nikiwa kama mbunge mwakilishi wa
wananchi nitakuwa mtu wa mwisho kufumbia macho uchakachuaji mkubwa
unaofanywa na baadhi ya makandarasi hao"
Alisema
hadi sasa ni kampuni moja pekee ya Boimanda ambayo imeonyesha uzalendo
wa kweli katika ujenzi wa barabara kwa kiwango cha changarawe katika
wilaya ya Ludewa ila makampuni yaliyosalia yamekuwa yakifanya
uchakachuaji mkubwa katika ujenzi huo na kuwa zaidi ya makampuni manne
ndio yanahusika na ujenzi huo kwa kila kampuni kupewa kipande.
Hivyo
alisema mara baada ya kurejea bungeni kwa kikao kijacho cha bunge moja
kati ya mambo ambayo atafikisha bungeni ni pamoja na shukrani kwa
kampuni ya Boimanda inayoongozwa na mkurugenzi wake Nicholaus Mgaya
kutokana na kuonyesha uwezo mkubwa wa kazi ila pia kufikisha kilio chake
dhidi ya makandarasi wabovu wanaoendelea na ujenzi huo.
Filikunjombe
alisema kasoro ambazo amepata kuziona kwa makandarasi hao ni pamoja na
kujenga barabara bila kuweka mifereji ya kupita maji ,kudanganya ujazo
wa kifusi kinachopaswa kumwagwa barabarani pamoja na mlazo mzuri wa
barabara baada ya kuchongwa .
Kwani
alisema iwapo kasoro hizo hazifanyiwa kazi basi ni wazi barabara hizo
hazitadumu na baada ya mvua kunyesha ni wazi Ludewa itarejea katika kero
yake ya mwanzo ya ubovu wa miundo mbinu.
Pia
alisema kwa mujibu wa mikataba makandarasi hao wanapaswa kukabidhi
barabara hizo tarehe 23 mwezi huu ila ukitazama ukubwa wa kazi iliyobaki
ni wazi kutakuwepo na ubabaishaji mkubwa katika kumalizia kazi hiyo kwa
ubora.
Wakati
huo huo mbunge huyo amempongeza Rais Dr Jakaya Kikwete kwa kutekeleza
ahadi yake kwa wana Ludewa juu ya uboreshaji wa barabara hizo kwa lengo
la kuwezesha wawekezaji wa madini ya liganga na Nchuchuma kufanikisha
kupitisha mitambo yao .
Alisema
kuwa uwajibikaji wa serikali iliyopo madarakani chini ya Rais Dr Kikwete
imekuwa ikileta matumaini makubwa kwa watanzania hasa wananchi wa jimbo
la Ludewa ambao kwa muda mrefu sasa hawajapata kuwa na barabara za lami
.
Aidha
alimpongeza waziri wa ujenzi Dr John Magufuli kwa kuendelea kuwa waziri
wa mfano katika baraza la mawaziri nchini kutokana na usimamizi mzuri wa
miradi ya barabara japo alisema wanaoendelea kumuangusha ni makandarasi
wasio wazalendo.
CHANZO:Francis Godwin